FMG Swahili Habari Siasa Michezo Udaku Mapenzi Biashara
Matangazo

Edo Kumwembe : Hii ni Aibu Kubwa Kwa Timu ya Simba


Edo Kumwembe : Hii ni Aibu Kubwa Kwa Timu ya Simba

“Sasa msimu umemalizika dhahiri kwa Simba. Sioni namna gani Simba wakichukua ubingwa kwa pengo la pointi lililopo. Baada ya Azam kucheza dakika 90 na za nyongeza dhidi ya Mashujaa bila ya kufunga bao lolote Ijumaa usiku sioni namna gani Yanga wanaweza kuzuiwa wasitwae ubingwa.


Swali ni namna gani Simba watarudi msimu ujao. Wamejifunza kitu au wataendelea kumdharau Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said? Watafumua kikosi chao cha utawala wa timu? Watarekebisha mipango yao ya usajili wa timu na kuleta wachezaji wenye hadhi ya Simba katika kikosi? Ni suala la kusubiri kwa sasa. .


Tupo Aprili. Mvua zinanyesha. Tusubiri Aprili ya mwakani kuona Simba itakuwa wapi. Kuona itakuwa imejirekebisha wapi. Leo ni aibu kuona baadhi ya mashabiki wa Simba wakiwa wanapumua baada ya kufungwa na Yanga. Kisa? Eti wamefungwa mabao machache kuliko walivyotazamia. Aibu.” — Edo Kumwembe.

Imeandikwa na Mbanga B
Powered by Blogger.